Quantcast
Channel: AMKA MTANZANIA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1010

ONGEA NA KOCHA; Kama Bilionea Akiishiwa Anaweza Kufanya Hivi, Kwa Nini Wewe Usianzie Hapa Na Ukafanikiwa?

$
0
0
Habari za leo rafiki yangu?

Karibu kwenye maongezi yetu ya siku ya leo, ambapo mimi kocha wako napata nafasi ya kukushirikisha mambo muhimu kuhakikisha maisha yako yanakuwa bora zaidi na unafanikiwa.
 

Leo nataka nikushirikishe habari moja niliyoisona na ikanisukuma sana kukushirikisha na wewe pia. Ni katika mahojiano ambapo Mjasiriamali Bilionea Mark Cuban aliulizwa swali kama akipoteza mali zake zote kwa pale alipo, je ataweza kurudi tena kwenye ubilionea?

Kabla sijakupa jibu lake ambalo lilinishangaza na kunifanya nikushikishe, naomba nikuambie kidogo kuhusu Mark Cuban na namna nilivyomfahamu.

SOMSA; Kama Unafikiri Huwezi Kuwa Bilionea Soma Hapa Na Uanze Kuelekea Kwenye Ubilionea.

Mark Cuban ni bilionea mjasiriamali wa nchini marekani. Amepata utajiri wake kutokana na shughuli za ujasiriamali, ambapo alianza na kampuni za mtandao wa intaneti baadaye akaweza kuuza kampuni zake na kuwa bilionea. Anawekeza kwenye makampuni mbalimbali na pia anamiliki timu ya mpira wa kikapu.

Nilimfahamu Mark Cuban kutokana na usomaji wangu wa vitabu, nilikutana na kitabu chake kinachoitwa How To Win At The Sport Of Business: If I Can Do It, You Can Do It.  

Kupitia kitabu hiki Cuban alitoa misingi 12 ya kila mjasiriamali kufuata kama anataka kufanikiwa. 

Unaweza kuzisoma sheria hizo kwenye makala hii; Sheria 12 Kwa Wanaoanza Biashara Kutoka Kwa Bilionea Mark Cuban. (bonyeza hayo maandishi kuisoma)

Sasa turudi kwenye jibu la swali aliloulizwa Cuban, iwapo anaweza kurudi kwenye ubilionea kama ikatokea amefilisika kabisa. Jibu lake lilikuwa na ndiyo na akasema hana wasiwasi kabisa kwamba atashindwa kuwa bilionea tena hata kama atapoteza kila kitu.

Alipoulizwa atawezaje kurudi kwenye ubilionea kama atapoteza kila kitu, na jibu lake ndiyo lilinishangaza ziadi.

SOMA; Orodha Mpya Ya Mabilionea; Mambo Kumi Ya Kuzingati Ili Na Wewe Uweze Kuingia Kwenye Orodha Hii Siku Za Baadae.

Alisema anajua uimara wake uko wapi, na hivyo atatafuta fursa mbili tu zitakazomrudisha kwenye ubilionea. Alisema atatafuta kazi ya kuwa mhudumu wa baa usiku na pia atatafuta kazi ya kuuza kwa kamisheni mchana. Hivyo mchana atakuwa anauza vitu kwa kamisheni na usiku atakuwa mhudumu wa baa. Anasema akifanya hivi kwa muda ataweza kutengeneza mtaji wa kumrudisha kwenye biashara na hatimaye kurudi kwenye utajiri.

Mark Cuban alijivunia ya kwamba anajua yupo vizuri kwenye mauzo, hivyo akipewa kitu chochote anaweza kukinadi na kumshawishi mtu akinunue. Kwa uimara huu alisema angetafuta bidhaa ambayo anaipenda na ina kamisheni kubwa, angepambana nayo mpaka aweze kupata akiba ya kumtosha kuanzisha biashara.

Najua unaweza kuwa unafikiria, ah anasema hivyo kwa sababu tayari ni bilionea, anaweza kusema chochote anachotaka. Ila nikuambie ya kwamba alianzia huko ndiyo akawa bilionea. 

Aliwahi kuwa mhudumu wa baa na wakati huo pia akiwa afisa mauzo wa kampuni ya kompyuta ambapo alipita nyumba kwa nyumba na ofisi kwa ofisi kuuza vifaa vya kompyuta.

SOMA; Jinsi Ya Kuondokana Na Hali Ya Kukosa Uthubutu Na Kuingia Kwenye Biashara Itakayokufikisha Kwenye Ubilionea.

Je unajifunza nini hapa rafiki yangu?

Sijakushirikisha tu habari hii ili ufurahie na kuhamasika, ila nimekushirikisha ili ujifunze na uchukue hatua mara moja kwenye maisha yako.

Na hii inaenda moja kwa moja kwa wale ambao wanasema wanataka kuanza biashara ila hawana mtaji. Badala ya kukaa na kusubiri mtaji, kwa nini usitafute shughuli yoyote unayoweza kufanya, hasa kuuza vitu kwa kamisheni na ukatengeneza mtaji wako hapo?

Hii pia inaenda moja kwa moja kwa wale wanaodharau kazi walizonazo sasa wakiona haziwafai na haziwezi kuwapeleka popote, kwa nini usianze kuitumia kazi hiyo kama njia ya wewe kutoka zaidi? Kwa nini usiweke juhudi kwa muda fulani na uweze kuondoka na kupiga hatua zaidi?

Mwisho kabisa napenda nikuambie rafiki yangu, acha kutafuta sababu za kujiridhisha na hali yoyote uliyonayo sasa. Acha kuwasingizia wazazi, ndugu na jamaa kwamba wamekutupa. Acha kupeleka lawama kwa serikali kwamba imeshindwa kukusaidia licha ya hilo kuwa jukumu la serikali. Ninachotaka kukuambia rafiki yangu, chukua hatua, waache wengine wajiridhishe watakavyo, ila wewe usicheze mchezo huo, chukua hatua na songa mbele.

Anzia chini kabisa, usiangalie wengine wanakuchukuliaje, usione watu watakuonaje na usomi wako, miaka ijayo watakuheshimu sana, na wengine watakuomba uwaajiri, kama tu hutafukia ndoto uliyonayo sasa. Nakusihi sana rafiki yangu, shika hatamu ya maisha yako kwenye mikono yako. Mwisho wa siku wewe ndiye unayeyaishi maisha yako, kama utataka kwa nje uonekane wa aina fulani lakini ndani ni wa tofauti, jua utajiumiza maisha yako yote.

Kila gumu unalopitia, litumie kama nafasi ya wewe kupiga hatua. Na popote ulipo sasa, hapo ndipo pa kuanzia. Kama serikali imekusomesha halafu sasa haikupi ajira, sawa, chukua hatua nyingine. Usiniambie umekaa unasubiri ajira miaka miwili na bado unaendelea kusubiri. Niambie kwamba unajipa miaka yako miwili ya kuchukua hatua hasa, bila ya kuangalia wengine wanasemaje, na nina uhakika utafika mbali sana. Kama umeweza kumudu miaka miwili bila ya ajira, utaweza kumudu mingine miwili ya kupambana kusimamisha maisha yako vizuri.

Kumbuka tupo pamoja kwenye safari hii rafiki, nipo hapa nilipo leo, nikikushirikisha maarifa haya, siyo kwa sababu serikali iliniambia hiyo ndiyo kazi yako, au kwa sababu wazazi, ndugu na jamaa waliniambia fanya hivyo, ila kwa sababu niliamua kushika hatamu ya maisha yangu, niliamua kupambana kuhakikisha maisha yangu yanasimama, na ninayaona matunda ya maamuzi haya kila siku. Ndiyo maana nina imani isiyo na shaka kabisa kwamba wewe rafiki yangu, iwapo utachukua hatua ya kushika hatamu ya maisha yako, hutabaki hapo ulipo sasa.

Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,

Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.

Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)

Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 1010

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>