Rafiki, karibu kwenye makala yetu ya leo ya ushauri wa changamoto mbalimbali ambazo zinatuzuia kufikia maisha ya mafanikio.
Leo tunakwenda kuangalia changamoto ya kutengeneza kipato kupitia uwezo na vipaji ambavyo tayari tunavyo au tunavyoweza kutengeneza.
Kabla hatujaingia ndani na kuona tunafanya nini, haya hapa ni maelezo ya msomaji mwenzetu aliyeomba ushauri kwenye hili;
Mimi nina kipaji cha kutype, nina speed kubwa sana na accuracy, ninafikiria kutafuta mashule mbalimbali ili niwe nawachapia mitihani yao. Changamoto kubwa ni namna nitakavyoweza kujitangaza ili nijulikane. Naomba ushauri wako tafadhali. Joyce M. M.
Joyce, hongera kwa kipaji hicho cha uchapaji ulicho nacho na pia vizuri sana kwa kufikiria namna gani unaweza kukitumia kutengeneza kipato ziadi. Kwa fikra hizi kama utachimba ndani zaidi utaona wazi hatua za kuchukua ili kuweza kutumia uwezo na vipaji vyako kutengeneza kipato.
Pamoja na kipaji hiki cha uchapaji ambacho unacho, bado hakikutoshelezi wewe kuweza kujitengenezea ajira itakayokupa kipato kizuri. Hii ni kwa sababu uwezo wa kuchapa pekee siyo kitu adimu sana. Kwani wachapaji wapo wengi.
SOMA; Jinsi Ya Kugundua Vipaji Vilivyopo Ndani Yako.
Unachopaswa kujua ni kwamba vitu adimu ndiyo vinavyopewa thamani kubwa. Kama kitu kinaweza kufanyika na watu wengi, basi hata thamani yake inakuwa ni ndogo. Hivyo uwezo wako wa kuchapa kwa kasi na kwa umakini, haukupi wewe kitu cha kujitofautisha na wengine wengi wanaoweza kufanya hivyo.
Hivyo ushauri mkubwa ninaokwenda kukupa leo ni kuongeza thamani yako kwa kuwa adimu zaidi. Na ili uwe adimu unahitaji kufanya vitu ambavyo haviwezi kufanywa na wengi.
Kwa kuwa tayari una uwezo wa kuchapa, sasa angalia vitu vingine unavyoweza kuviongezea kwenye uchapaji ili uwe adimu zaidi.
Kwa mfano unaweza kujifunza uandishi wa vitabu na makala na kuanza kuandika, kwa kuwa una kasi na umakini mkubwa, utaweza kuzalisha kazi nyingi zinazoweza kuwasaidia watu na wao wakawa tayari kukulipa.
Pia unaweza kujifunza uhariri na kuwasaidia watu kuhariri kazi zao na wakakulipa. Kwa kuwa una kasi na umakini, unaweza kupitia kazi kubwa za watu, kuzirekebisha na wao wakakulipa.
SOMA; Jinsi ya kugeuza kipaji chako kuwa biashara inayokuingizia kipato.
Pia unaweza kuwafundisha watu namna ya kuongeza kasi kwenye uchapaji. Ni namna gani wewe uliweza kuwa na kasi na umakini? Wapo wengi ambao wangependa kuweza kuchapa kwa kasi na umakini mkubwa na wapo tayari kulipia ili kufundishwa.
Pia unaweza kuwasaidia watu kuandika vitabu au makala. Wapo watu ambao wana mawazo mazuri ambayo yangefaa kuwa kitabu au makala nzuri lakini hawana muda na uwezo wa kubadili mawazo hayo kwenda kwenye maandishi. Wewe unaweza kuwasaidia hilo nakutengeneza kipato.
Kama tulivyoona hapo juu, zipo njia nyingi za kuongeza thamani kwenye uwezo wako wa kuchapa ili kuweza kutengeneza kipato kupitia uwezo na kipaji chako.
Sasa swali la msingi ni je unawezaje kuwafikia watu unaoweza kufanya nao kazi?
Jibu ni kwa kuwaonesha kazi zako ambazo tayari umeshafanya. Na hapa unahitaji kuwa na kazi ambazo tayari umeshawafanyia wengine na wapo tayari kutoa ushuhuda mzuri, au unahitaji kuwa na eneo lenye kazi zako kama vile blog.
SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutumia Saa Hili moja Kufikia Mafanikio Makubwa.
Hivyo kitu cha kwanza kabisa nakushauri uanzishe blog yako na chagua mada utakayokuwa unaandikia. Katika maelezo ya blog yako eleza huduma ambazo utakuwa unatoa, ikiwepo ya uchapaji na uhariri wa vitabu na makala. Wakati huo unaendelea kujifunza na kuboresha ujuzi na vipaji vyako vingine ili baadaye uweze kutoa thamani kubwa zaidi.
Unaweza pia kuanza kwa kuwasaidia watu kazi zao bure kabisa na hapa ukaonesha uwezo ambao upo ndani yako. baada ya huduma hiyo ya bure, baadaye watakapohitaji ndiyo watalipia kulingana na gharama zako.
Kwa Joyce na marafiki wengine, kutegemea kipaji au uwezo mmoja pekee katika kutengeneza kipato, ili hali kitu hicho kila mtu anaweza kukifanya ni kujidanganya. Utakosa thamani kubwa ya kutoa kwa wengine na hivyo kushindwa kutengeneza kipato kizuri.
Ongeza zaidi ujuzi na jua zaidi vipaji vilivyopo ndani yako. kadiri unavyoweza kuleta pamoja vitu vidogo vidogo unavyoweza kufanya na vinavyoendana, ndivyo unavyoongeza thamani yako na kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kutengeneza kipato kupitia ujuzi na vipaji vyako.
Nakutakia utekelezaji mwema wa yale ambayo umejifunza,
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani
makirita@kisimachamaarifa.co.tz
TOA CHANGAMOTO YAKO USHAURIWE
Kama una changamoto ambayo inakuzuia kufikia malengo yako unaweza kuitoa kwa kubonyeza maandishi haya na kujaza fomu. Changamoto yako inaweza kuwa moja ya makala zijazo kila siku ya jumatatu.
Kama ungependa kupata ushauri wa moja kwa moja kutoka kwangu kuhusiana na changamoto yako bonyeza maandishi haya na utapata utaratibu wa kupata ushauri kutoka kwangu. Karibu sana rafiki tufanye kazi kwa pamoja.
Kupata vitabu vya mafanikio kwenye Kazi, Biashara Na Maisha kwa ujumla tembelea MOBILE UNIVERSITY, bonyeza hayo maandishi.
Leo tunakwenda kuangalia changamoto ya kutengeneza kipato kupitia uwezo na vipaji ambavyo tayari tunavyo au tunavyoweza kutengeneza.
Kabla hatujaingia ndani na kuona tunafanya nini, haya hapa ni maelezo ya msomaji mwenzetu aliyeomba ushauri kwenye hili;
Mimi nina kipaji cha kutype, nina speed kubwa sana na accuracy, ninafikiria kutafuta mashule mbalimbali ili niwe nawachapia mitihani yao. Changamoto kubwa ni namna nitakavyoweza kujitangaza ili nijulikane. Naomba ushauri wako tafadhali. Joyce M. M.
Joyce, hongera kwa kipaji hicho cha uchapaji ulicho nacho na pia vizuri sana kwa kufikiria namna gani unaweza kukitumia kutengeneza kipato ziadi. Kwa fikra hizi kama utachimba ndani zaidi utaona wazi hatua za kuchukua ili kuweza kutumia uwezo na vipaji vyako kutengeneza kipato.
Pamoja na kipaji hiki cha uchapaji ambacho unacho, bado hakikutoshelezi wewe kuweza kujitengenezea ajira itakayokupa kipato kizuri. Hii ni kwa sababu uwezo wa kuchapa pekee siyo kitu adimu sana. Kwani wachapaji wapo wengi.
SOMA; Jinsi Ya Kugundua Vipaji Vilivyopo Ndani Yako.
Unachopaswa kujua ni kwamba vitu adimu ndiyo vinavyopewa thamani kubwa. Kama kitu kinaweza kufanyika na watu wengi, basi hata thamani yake inakuwa ni ndogo. Hivyo uwezo wako wa kuchapa kwa kasi na kwa umakini, haukupi wewe kitu cha kujitofautisha na wengine wengi wanaoweza kufanya hivyo.
Hivyo ushauri mkubwa ninaokwenda kukupa leo ni kuongeza thamani yako kwa kuwa adimu zaidi. Na ili uwe adimu unahitaji kufanya vitu ambavyo haviwezi kufanywa na wengi.
Kwa kuwa tayari una uwezo wa kuchapa, sasa angalia vitu vingine unavyoweza kuviongezea kwenye uchapaji ili uwe adimu zaidi.
Kwa mfano unaweza kujifunza uandishi wa vitabu na makala na kuanza kuandika, kwa kuwa una kasi na umakini mkubwa, utaweza kuzalisha kazi nyingi zinazoweza kuwasaidia watu na wao wakawa tayari kukulipa.
Pia unaweza kujifunza uhariri na kuwasaidia watu kuhariri kazi zao na wakakulipa. Kwa kuwa una kasi na umakini, unaweza kupitia kazi kubwa za watu, kuzirekebisha na wao wakakulipa.
SOMA; Jinsi ya kugeuza kipaji chako kuwa biashara inayokuingizia kipato.
Pia unaweza kuwafundisha watu namna ya kuongeza kasi kwenye uchapaji. Ni namna gani wewe uliweza kuwa na kasi na umakini? Wapo wengi ambao wangependa kuweza kuchapa kwa kasi na umakini mkubwa na wapo tayari kulipia ili kufundishwa.
Pia unaweza kuwasaidia watu kuandika vitabu au makala. Wapo watu ambao wana mawazo mazuri ambayo yangefaa kuwa kitabu au makala nzuri lakini hawana muda na uwezo wa kubadili mawazo hayo kwenda kwenye maandishi. Wewe unaweza kuwasaidia hilo nakutengeneza kipato.
Kama tulivyoona hapo juu, zipo njia nyingi za kuongeza thamani kwenye uwezo wako wa kuchapa ili kuweza kutengeneza kipato kupitia uwezo na kipaji chako.
Sasa swali la msingi ni je unawezaje kuwafikia watu unaoweza kufanya nao kazi?
Jibu ni kwa kuwaonesha kazi zako ambazo tayari umeshafanya. Na hapa unahitaji kuwa na kazi ambazo tayari umeshawafanyia wengine na wapo tayari kutoa ushuhuda mzuri, au unahitaji kuwa na eneo lenye kazi zako kama vile blog.
SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kutumia Saa Hili moja Kufikia Mafanikio Makubwa.
Hivyo kitu cha kwanza kabisa nakushauri uanzishe blog yako na chagua mada utakayokuwa unaandikia. Katika maelezo ya blog yako eleza huduma ambazo utakuwa unatoa, ikiwepo ya uchapaji na uhariri wa vitabu na makala. Wakati huo unaendelea kujifunza na kuboresha ujuzi na vipaji vyako vingine ili baadaye uweze kutoa thamani kubwa zaidi.
Unaweza pia kuanza kwa kuwasaidia watu kazi zao bure kabisa na hapa ukaonesha uwezo ambao upo ndani yako. baada ya huduma hiyo ya bure, baadaye watakapohitaji ndiyo watalipia kulingana na gharama zako.
Kwa Joyce na marafiki wengine, kutegemea kipaji au uwezo mmoja pekee katika kutengeneza kipato, ili hali kitu hicho kila mtu anaweza kukifanya ni kujidanganya. Utakosa thamani kubwa ya kutoa kwa wengine na hivyo kushindwa kutengeneza kipato kizuri.
Ongeza zaidi ujuzi na jua zaidi vipaji vilivyopo ndani yako. kadiri unavyoweza kuleta pamoja vitu vidogo vidogo unavyoweza kufanya na vinavyoendana, ndivyo unavyoongeza thamani yako na kujiweka kwenye mazingira mazuri ya kutengeneza kipato kupitia ujuzi na vipaji vyako.
Nakutakia utekelezaji mwema wa yale ambayo umejifunza,
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani
makirita@kisimachamaarifa.co.tz
TOA CHANGAMOTO YAKO USHAURIWE
Kama una changamoto ambayo inakuzuia kufikia malengo yako unaweza kuitoa kwa kubonyeza maandishi haya na kujaza fomu. Changamoto yako inaweza kuwa moja ya makala zijazo kila siku ya jumatatu.
Kama ungependa kupata ushauri wa moja kwa moja kutoka kwangu kuhusiana na changamoto yako bonyeza maandishi haya na utapata utaratibu wa kupata ushauri kutoka kwangu. Karibu sana rafiki tufanye kazi kwa pamoja.
Kupata vitabu vya mafanikio kwenye Kazi, Biashara Na Maisha kwa ujumla tembelea MOBILE UNIVERSITY, bonyeza hayo maandishi.