Habari za leo rafiki?
Kama wewe ni mtumiaji wa mtandao wa intaneti, utakuwa umeshawahi kupokea ujumbe unaokuambia kwamba kuna njia unaweza kutengeneza mamilioni ya fedha kupitia mtandao wa intaneti, bila ya kufanya kazi kubwa. Jumbe hizi zinakuwa na ushawishi sana wa kutaka kujaribu kile ambacho watu wamekuwa wanaambiwa.
Na ushawishi zaidi unatolewa na watu wanaodai kwamba wameshatengeneza kipato cha aina hiyo na kuonesha mchakato mzima wanaotumia wao na kipato walichotengeneza. Watu wamekuwa wakitamani kuchukua hatua hizo ili na wao waweze kutengeneza kipato hicho, lakini wanakutana na jukumu moja wanalopaswa kufanya. Na jukumu hilo ni kusambaza ujumbe wa kwamba mtu anaweza kutengeneza kipato kikubwa kwenye mtandao.
Kwa kuwa watu wana tamaa ya fedha, wanatuma ujumbe ule ili wapate fedha hizo, na hilo ndiyo linapelekea wewe kupokea ujumbe kwa watu wako wa karibu, wakikuambia fungua link fulani na utaweza kutengeneza mamilioni ya fedha. Ukifungua na wewe unaambiwa utume kwa wengi na mchezo unaendelea hivyo.
Kwenye kipindi cha leo nimelijadili hili kwa kina, uwezekano wa kutengeneza mamilioni kwenye intaneti na nini unapaswa kufanya ili kuweza kutengeneza kipato hicho.
Kabla hujakimbilia kutafuta hizo link za kutengeneza mamilioni kwenye intaneti, nakushauri sana uangalie kipindi hichi, kitakupa mwanga na hatua za kuchukua.
Kuangalia kipindi hichi cha leo bonyeza maandishi haya. Pia unaweza kukiangalia kipindi hichi moja kwa moja hapo chini.
Usikubali kudanganyika kwa namba yoyote ile, ijue misingi sahihi ya kutengeneza fedha kwenye intaneti kisha chukua hatua sahihi.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Kupata blog yako ya kitaalamu, unayoweza kuitumia kutengeneza kipato, BONYEZA maandishi haya.
Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea www.kisimachamaarifa.co.tz/vitabu
Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.