Habari za leo rafiki yangu?
Mwaka 2017 unakwendaje kwako?
Unachukua hatua au bado unalalamika?
Kama unachukua hatua basi hongera sana, kwa sababu ni kuchukua hatua pekee ndipo kutakapokuletea matokeo ambayo unayataka. Kuchukua hatua kutakutoa hapo ulipo sasa na kukufikisha mbele zaidi, hata kama ni padogo.
Kama bado unalalamika, unalalamikia serikali, unawalalamikia ndugu na jamaa, unamlalamikia mwajiri, basi nikupe pole kwa sababu umechagua njia ambayo haina majibu. Yaani umechagua kufanya kitu ambacho hakina uzalishaji, ni sawa na kusukuma ukuta kwa mikono, unaweza kutokwa jasho na kuchoka kabisa, lakini hakuna kazi ambayo unakuwa umefanya. Kwenye fizikia wanasema WORK DONE IS ZERO, yaani kama umesukuma kitu lakini hakijasogea, hujafanya kazi. Kifizikia kazi inapimwa kwa kiwango ambacho imesogea. Hivyo kulalamika, hata kama upo sahihi kabisa, hujafanya kazi yoyote, kwa sababu kulalamika ni kuongea tu, na maneno hayaleti mabadiliko hata siku moja, ni VITENDO.
Leo nataka kuandika vitu ambavyo sijaandika siku nyingi na ambavyo naona watu wengi wanavifanya kimakosa huku wakitegemea matokeo makubwa sana. Wengine wamekuwa wanashindwa kuanza kwa kujipa sababu lukuki, lakini ukweli ni kwamba hawana kile wanachopaswa kuwa nacho ili kupiga hatua.
SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuwa Jasiri Na Kufanya Mambo Makubwa Zaidi Ya Unavyofikiria.
Watu wengi wamekuwa wanalalamika kwamba maisha ni magumu, fedha hakuna na mambo hayaendi, lakini ukweli ni kwamba wengi wamechagua yale maisha wanayoishi sasa, yaani watu wamechagua maisha ambayo ni magumu zaidi, wamechagua maisha ambayo hakuna fedha na wamechagua mambo kutokwenda. Hii ndiyo maana pekee ya malalamiko haya kwenye karne hii ya 21 ambapo kila mtu ana uhuru wa kufanya chochote anachotaka kufanya kama hakivunji sheria.
Lakini watu wengi wamekuwa hawachukui hatua, badala yake wanaendelea kukaa pale walipo, na kuendelea kufanya kile wanachofanya, huku wakiendelea kulalamika kwamba mambo hayaendi.
Albert Einstein amewahi kunukuliwa akisema kwamba ujinga ni kufanya jambo lile lile, kwa njia ile ile na kutegemea kupata matokeo tofauti. Sasa hapa ndipo ninapotaka na wewe ufikirie.
Kwamba umekuwa unafanya mambo yale yale, mwaka nenda mwaka rudi. Unaenda kazini na kufanya kazi zako vile vile, unapokea mshahara ambao haukutoshi, unaenda kukopa na ukipokea mshahara mwingine unalipa madeni. Unaenda hivi miaka mitano, kumi mpaka sihirini, halafu ndani yako unafikiria kabisa kuna muujiza utakaotokea na kubadili mambo?
Unafanya biashara yako vile vile, huduma na bidhaa unazotoa ni zile zile, wateja ulionao ni wale wale na hakuna kipya kikubwa unachofanya, halafu unataka kutuaminisha kwamba mambo ni magumu kwako? Ndiyo tutaamini mambo ni magumu kwako, na tuna uhakika ni magumu kwa sababu umechagua na umeridhika na mambo hayo.
Kila kitu ambacho unafanya sasa, unafanya hivyo kwa sababu umechagua wewe mwenyewe, au umeridhika na kitu hicho, vinginevyo ungeshaondoka zamani sana. Naomba nirudie hili kwa msisitizo zaidi. UPO HAPO ULIPO, UKIFANYA HICHO UNACHOFANYA, KWA SABABU UMECHAGUA KUKIFANYA AU UMERIDHIKA NA MATOKEO AMBAYO UNAPATA. INGEKUWA HUJARIDHIKA UNGESHAFANYA KILA MBINU UTOKE HAPO ULIPO SASA.
Najua kuna ambao wamenasa, yaani wanataka kutoka lakini wanaona hawawezi kutoka, wamenasa. Kama vile ambavyo mtu yupo kwenye kazi ambayo haipendi na wala haimlipi vizuri lakini hawezi kuiacha kwa sababu ndiyo anaitegemea kuendesha familia yake. Naelewa vizuri sana kwamba kuna uwezekano umenasa, unatamani sana kutoka lakini ukiangalia nyuma huthubutu kufanya hivyo.
Leo nataka kuongea na wale ambao wamenasa, wale ambao wamechoka lakini hawaoni wanatokaje pale walipo. Wale ambao wanatamani sana kupiga hatua lakini hawaoni wapi waanzie. Na hata ndiyo ninayotaka kuwapa siku ya leo.
SOMA; Kama Una Tabia Sugu Inayokukera Iondoe Hivi.
MAPENZI.
Ni kitu gani unakipenda sana kwenye maisha yako, kitu gani unapenda sana kuhusu maisha yako na kitu gani ambacho unapenda kufuatilia na kitu gani ambacho unapenda kuongelea na kushirikisha wengine?
Kuna mwanamuziki siku za nyuma kidogo aliwahi kuimba wimbo unaitwa MAPENZI YANA RUN DUNIA, akimaanisha mapenzi ndiyo yanaendesha dunia. Na hii ni kweli kabisa, siyo tu kwa mapenzi kati ya wachumba au wenza, bali mapenzi kwa ujumla.
Wale wanaofanikiwa sana ni wale ambao wana mapenzi makubwa kwenye kile ambacho wanakifanya. Wale ambao hakuna namna unaweza kuwatoa kwenye kile wanachofanya, kwa sababu kimeshakuwa sehemu ya maisha yako.
Hivyo na wewe, tafuta kitu ambacho unakipenda sana, kitu ambacho upo tayari kukifanya na kukisimamia hata kama kila mtu anafanya tofauti au anakushangaa. Na anza kukifanya, wakati unaendelea kufanya kile unachofanya sasa, na hapo utapata ukombozi wako.
Mapenzi yana nguvu kubwa sana, angalia namna watu wanavyoweza kufanya mambo ya ajabu kabisa kwa ajili ya mapenzi, sasa wewe tumia nguvu hivyo vizuri ili uweze kutoka hapo ulipo sasa.
HASIRA.
Ni kitu gani ambacho kinakukasirisha sana kuhusu maisha yako na hata kwenye maisha yako. Ni kitu gani ambacho huwezi kukivumilia kabia, kila unapokiona hupati amani kabisa, yaani unatamani kufanya kitu ili kubadili ile hali inayokupa hasira?
Hapa ndipo ilipo nguvu nyingine ya kukuwezesha wewe kutoka hapo ulipo sasa. Iwe umeridhika tu au umenasa, kwa kupata hasira ambayo huwezi kuivumilia, itakusukuma kuchukua hatua kubwa.
Hasira tunayojadili hapa siyo ya kugombana na watu au kupiga watu, bali hasira ya kuchoka na namna maisha yanavyokwenda, hasira ya kutaka mambo yawe bora zaidi. Hasira ya kukufanya usiwe mzembe, uwe tayari kuchukua hatua hata kama wengine hawachukui hatua.
KUJITOA.
Ni kitu gani upo tayari kujitoa mhanga kwa ajili ya hicho kwenye maisha yako. Ni wapi upo tayari kwenda hatua ya ziada, kufanya zaidi ya wengine na hata kuwasaidia watu zaidi? Ni eneo gani la maisha yako ambapo hijibanii, upo tayari kutoa zaidi, upo tayari kuwanufaisha watu zaidi?
Kiwango chako cha kujitoa ndiyo kinachokutofautisha na wengine na ndiyo kitakachokutoa hapo ulipo sasa.
SOMA; Kuanza Biashara Kwa Mtaji Kidogo, Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Ili Kuikuza.
KUPAMBANA.
Mambo hayatakuwa rahisi, utasoma hapa, utapata hamasa na kusema yaani kuanzia leo nabadili maisha yangu kabisa, nitafanya haya muhimu kila siku. Lakini kesho utaamka ukiwa na mawazo ya changamoto zako nyingine na kuwa umesahau haya kabisa. Au utaanza kuyafanya na watu wanaanza kukushangaa, wengine wanakupinga, wengine wanakusema vibaya, wengine wanakukatisha tamaa.
Napenda nikuambie wazi kabisa, mambo hayatakuwa rahisi na hivyo utahitaji kupambana sana, yaani SANA. Utahitaji kupambana siyo kidogo. Kupambana na uzembe na uvivu wako mwenyewe, kupambana na wale wanaokuzunguka na kupambana na changamoto zinazotokana na kile unachofanya.
Hivyo ndivyo unavyoweza kutoka hapo ulipo nasa rafiki yangu. Hizo ndizo hatua zitakazokutoa hapo, zifanyie kazi na utoke, au achana nazo na uendelee kulalamika. Lakini kabla hujaendelea kulalamika, fanya tathmini tangu umeanza kulalamika, ni matokeo gani makubwa umewahi kuyapata kwenye maisha yako kutokana na kulalamika?
Usikubali kuwa mjinga, kwa kufanya mambo yale yale na kutegemea matokeo tofauti. Kuwa mwerevu na chukua hatua sasa. Na hatua za kuanza kuchukua kuanzia leo tayari nimeshakupa hapo. Kazi ni kwako tu rafiki yangu.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)
Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.
Mwaka 2017 unakwendaje kwako?
Unachukua hatua au bado unalalamika?
Kama unachukua hatua basi hongera sana, kwa sababu ni kuchukua hatua pekee ndipo kutakapokuletea matokeo ambayo unayataka. Kuchukua hatua kutakutoa hapo ulipo sasa na kukufikisha mbele zaidi, hata kama ni padogo.
Kama bado unalalamika, unalalamikia serikali, unawalalamikia ndugu na jamaa, unamlalamikia mwajiri, basi nikupe pole kwa sababu umechagua njia ambayo haina majibu. Yaani umechagua kufanya kitu ambacho hakina uzalishaji, ni sawa na kusukuma ukuta kwa mikono, unaweza kutokwa jasho na kuchoka kabisa, lakini hakuna kazi ambayo unakuwa umefanya. Kwenye fizikia wanasema WORK DONE IS ZERO, yaani kama umesukuma kitu lakini hakijasogea, hujafanya kazi. Kifizikia kazi inapimwa kwa kiwango ambacho imesogea. Hivyo kulalamika, hata kama upo sahihi kabisa, hujafanya kazi yoyote, kwa sababu kulalamika ni kuongea tu, na maneno hayaleti mabadiliko hata siku moja, ni VITENDO.
Leo nataka kuandika vitu ambavyo sijaandika siku nyingi na ambavyo naona watu wengi wanavifanya kimakosa huku wakitegemea matokeo makubwa sana. Wengine wamekuwa wanashindwa kuanza kwa kujipa sababu lukuki, lakini ukweli ni kwamba hawana kile wanachopaswa kuwa nacho ili kupiga hatua.
SOMA; Hivi Ndivyo Unavyoweza Kuwa Jasiri Na Kufanya Mambo Makubwa Zaidi Ya Unavyofikiria.
Watu wengi wamekuwa wanalalamika kwamba maisha ni magumu, fedha hakuna na mambo hayaendi, lakini ukweli ni kwamba wengi wamechagua yale maisha wanayoishi sasa, yaani watu wamechagua maisha ambayo ni magumu zaidi, wamechagua maisha ambayo hakuna fedha na wamechagua mambo kutokwenda. Hii ndiyo maana pekee ya malalamiko haya kwenye karne hii ya 21 ambapo kila mtu ana uhuru wa kufanya chochote anachotaka kufanya kama hakivunji sheria.
Lakini watu wengi wamekuwa hawachukui hatua, badala yake wanaendelea kukaa pale walipo, na kuendelea kufanya kile wanachofanya, huku wakiendelea kulalamika kwamba mambo hayaendi.
Albert Einstein amewahi kunukuliwa akisema kwamba ujinga ni kufanya jambo lile lile, kwa njia ile ile na kutegemea kupata matokeo tofauti. Sasa hapa ndipo ninapotaka na wewe ufikirie.
Kwamba umekuwa unafanya mambo yale yale, mwaka nenda mwaka rudi. Unaenda kazini na kufanya kazi zako vile vile, unapokea mshahara ambao haukutoshi, unaenda kukopa na ukipokea mshahara mwingine unalipa madeni. Unaenda hivi miaka mitano, kumi mpaka sihirini, halafu ndani yako unafikiria kabisa kuna muujiza utakaotokea na kubadili mambo?
Unafanya biashara yako vile vile, huduma na bidhaa unazotoa ni zile zile, wateja ulionao ni wale wale na hakuna kipya kikubwa unachofanya, halafu unataka kutuaminisha kwamba mambo ni magumu kwako? Ndiyo tutaamini mambo ni magumu kwako, na tuna uhakika ni magumu kwa sababu umechagua na umeridhika na mambo hayo.
Kila kitu ambacho unafanya sasa, unafanya hivyo kwa sababu umechagua wewe mwenyewe, au umeridhika na kitu hicho, vinginevyo ungeshaondoka zamani sana. Naomba nirudie hili kwa msisitizo zaidi. UPO HAPO ULIPO, UKIFANYA HICHO UNACHOFANYA, KWA SABABU UMECHAGUA KUKIFANYA AU UMERIDHIKA NA MATOKEO AMBAYO UNAPATA. INGEKUWA HUJARIDHIKA UNGESHAFANYA KILA MBINU UTOKE HAPO ULIPO SASA.
Najua kuna ambao wamenasa, yaani wanataka kutoka lakini wanaona hawawezi kutoka, wamenasa. Kama vile ambavyo mtu yupo kwenye kazi ambayo haipendi na wala haimlipi vizuri lakini hawezi kuiacha kwa sababu ndiyo anaitegemea kuendesha familia yake. Naelewa vizuri sana kwamba kuna uwezekano umenasa, unatamani sana kutoka lakini ukiangalia nyuma huthubutu kufanya hivyo.
Leo nataka kuongea na wale ambao wamenasa, wale ambao wamechoka lakini hawaoni wanatokaje pale walipo. Wale ambao wanatamani sana kupiga hatua lakini hawaoni wapi waanzie. Na hata ndiyo ninayotaka kuwapa siku ya leo.
SOMA; Kama Una Tabia Sugu Inayokukera Iondoe Hivi.
MAPENZI.
Ni kitu gani unakipenda sana kwenye maisha yako, kitu gani unapenda sana kuhusu maisha yako na kitu gani ambacho unapenda kufuatilia na kitu gani ambacho unapenda kuongelea na kushirikisha wengine?
Kuna mwanamuziki siku za nyuma kidogo aliwahi kuimba wimbo unaitwa MAPENZI YANA RUN DUNIA, akimaanisha mapenzi ndiyo yanaendesha dunia. Na hii ni kweli kabisa, siyo tu kwa mapenzi kati ya wachumba au wenza, bali mapenzi kwa ujumla.
Wale wanaofanikiwa sana ni wale ambao wana mapenzi makubwa kwenye kile ambacho wanakifanya. Wale ambao hakuna namna unaweza kuwatoa kwenye kile wanachofanya, kwa sababu kimeshakuwa sehemu ya maisha yako.
Hivyo na wewe, tafuta kitu ambacho unakipenda sana, kitu ambacho upo tayari kukifanya na kukisimamia hata kama kila mtu anafanya tofauti au anakushangaa. Na anza kukifanya, wakati unaendelea kufanya kile unachofanya sasa, na hapo utapata ukombozi wako.
Mapenzi yana nguvu kubwa sana, angalia namna watu wanavyoweza kufanya mambo ya ajabu kabisa kwa ajili ya mapenzi, sasa wewe tumia nguvu hivyo vizuri ili uweze kutoka hapo ulipo sasa.
HASIRA.
Ni kitu gani ambacho kinakukasirisha sana kuhusu maisha yako na hata kwenye maisha yako. Ni kitu gani ambacho huwezi kukivumilia kabia, kila unapokiona hupati amani kabisa, yaani unatamani kufanya kitu ili kubadili ile hali inayokupa hasira?
Hapa ndipo ilipo nguvu nyingine ya kukuwezesha wewe kutoka hapo ulipo sasa. Iwe umeridhika tu au umenasa, kwa kupata hasira ambayo huwezi kuivumilia, itakusukuma kuchukua hatua kubwa.
Hasira tunayojadili hapa siyo ya kugombana na watu au kupiga watu, bali hasira ya kuchoka na namna maisha yanavyokwenda, hasira ya kutaka mambo yawe bora zaidi. Hasira ya kukufanya usiwe mzembe, uwe tayari kuchukua hatua hata kama wengine hawachukui hatua.
KUJITOA.
Ni kitu gani upo tayari kujitoa mhanga kwa ajili ya hicho kwenye maisha yako. Ni wapi upo tayari kwenda hatua ya ziada, kufanya zaidi ya wengine na hata kuwasaidia watu zaidi? Ni eneo gani la maisha yako ambapo hijibanii, upo tayari kutoa zaidi, upo tayari kuwanufaisha watu zaidi?
Kiwango chako cha kujitoa ndiyo kinachokutofautisha na wengine na ndiyo kitakachokutoa hapo ulipo sasa.
SOMA; Kuanza Biashara Kwa Mtaji Kidogo, Mambo Muhimu Ya Kuzingatia Ili Kuikuza.
KUPAMBANA.
Mambo hayatakuwa rahisi, utasoma hapa, utapata hamasa na kusema yaani kuanzia leo nabadili maisha yangu kabisa, nitafanya haya muhimu kila siku. Lakini kesho utaamka ukiwa na mawazo ya changamoto zako nyingine na kuwa umesahau haya kabisa. Au utaanza kuyafanya na watu wanaanza kukushangaa, wengine wanakupinga, wengine wanakusema vibaya, wengine wanakukatisha tamaa.
Napenda nikuambie wazi kabisa, mambo hayatakuwa rahisi na hivyo utahitaji kupambana sana, yaani SANA. Utahitaji kupambana siyo kidogo. Kupambana na uzembe na uvivu wako mwenyewe, kupambana na wale wanaokuzunguka na kupambana na changamoto zinazotokana na kile unachofanya.
Hivyo ndivyo unavyoweza kutoka hapo ulipo nasa rafiki yangu. Hizo ndizo hatua zitakazokutoa hapo, zifanyie kazi na utoke, au achana nazo na uendelee kulalamika. Lakini kabla hujaendelea kulalamika, fanya tathmini tangu umeanza kulalamika, ni matokeo gani makubwa umewahi kuyapata kwenye maisha yako kutokana na kulalamika?
Usikubali kuwa mjinga, kwa kufanya mambo yale yale na kutegemea matokeo tofauti. Kuwa mwerevu na chukua hatua sasa. Na hatua za kuanza kuchukua kuanzia leo tayari nimeshakupa hapo. Kazi ni kwako tu rafiki yangu.
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku. Bonyeza maandishi haya kujiunga na KISIMA CHA MAARIFA.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)
Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.