Rafiki,
Katikati ya mwaka 2014 nilipata maono (VISION) ya kusoma vitabu 500 ndani ya miaka mitano. Hakika haya yalikuwa maono makubwa ambayo sikuwahi kufikiri kama yanawezekana. Hivyo sikuanza kuyafanyia kazi mara moja, bali nilikaa chini nikifikiria inawezekanaje kufikia maono hayo makubwa. Mwenyewe nilipata wasiwasi kama itawezekana. Kwa wakati huo nilikuwa tayari nina miaka miwili ya usomaji wa vitabu, lakini sikuwa nimesoma vitabu vingi sana ndani ya miaka hiyo miwili.
Siku moja nikiwa na maongezi na rafiki yangu Daudi Mwakalinga nikamshirikisha hili, na akalipokea akawa chanya sana kwenye hili. Nikaona kumbe inawezekana. Basi nikakaa chini na kupiga mahesabu, vitabu 500 ndani ya miaka mitano vinaishaje?
Nikagundua inabidi kusoma vitabu 100 kila mwaka, hivyo miaka mitano vitakuwa vitabu 500.
Nikaendelea na hesabu zangu, kama mwaka ninahitaji kusoma vitabu 100, je nitavigawaje hivyo vitabu 100. Nikaona kwa mwaka kuna wiki 52, hivyo kama nitasoma vitabu viwili kila siku, kwa mwaka vitakuwa vitabu 104, nikaona hapa sasa namba inahesabika. Vitabu viwili kila wiki, siyo mzigo mkubwa sana, angalau ni kitu kinachowezekana kufanyika.
Kufika Oktoba mwaka huo 2014 nilikuja na mpango wa kuanzisha kundi la kusoma vitabu, kwa sababu nilijua kama nataka kufikia lengo hili, basi ni vyema nikaenda na wale wanaoweza kwenda.
Kwa kuwa mimi huwa napenda kufanya mambo magumu yawe rahisi, nikasema inabidi kutengeneza kundi ambalo litakuwa na watu wanaopenda kusoma vitabu, na lisiongeze mzigo kwa mtu. Mfano ulazima wa kukutana mara kwa mara na mengine ambayo yangeweza kuzuia au kuleta changamoto kwenye usomaji wetu wa vitabu.
Hivyo nikaona njia rahisi ni kutumia teknolojia mpya zinazokuja kila siku. Hivyo nikaamua kuanzisha kundi kupitia mtandao wa TELEGRAM, wakati huo wasap ilikuwa bado hamwezi kutumiana vitabu, lakini telegram itafaa. Na nikaweka mpango kwamba tutakuwa na kundi la kusoma vitabu, ambapo shughuli pekee ni usomaji wa vitabu, na siku moja ya wiki kila mtu LAZIMA ashirikishe kile ambacho amesoma kwenye vitabu, na kwa kila kitabu ashirikishe mambo 20 aliyojifunza. Kushindwa kufanya hivyo zaidi ya wiki mbili mtu huyo anatolewa.
Basi baada ya kuona mpango huu ni mwema, ndipo nilipoandika na kutoa taarifa kwa watanzania wenzangu kupitia mtandao wa AMKA MTANZANIA. Nilijua taarifa hii ingepokelewa vizuri na kwa hamasa, lakini mambo yalikuwa tofauti. Wengi walisema haiwezekani, walipinga mno na kushangaa kabisa. lakini nashukuru kuna watu kama 50 kwa kipindi kile waliitikia wito na tukaanza kusoma vitabu.
Hapa ndipo TANZANIA VORACIOUS READERS() ilipozaliwa. Kundi la kusoma vitabu ambalo kila mtu anakaribishwa kujiunga bure kabisa, lakini asipotimiza wajibu wa kusoma vitabu na kushirikisha wengine yale aliyojifunza anaondolewa. Tangu kipindi hicho tumekuwa tunasoma vitabu viwili kila wiki na tumekuwa tunaongezeka na kupungua kulingana na watu kuweza kuendana na taratibu za kikundi.
Wapo watu walioondolewa kwenye kundi na kulalamika mno, na wakati utaratibu ulikuwa wazi kabisa kwamba usipotimiza mahitaji ya kundi la usomaji wa vitabu utaondolewa.
Ninachoweza kusema ni kwamba kwa zaidi ya miaka hii miwili ya kusoma vitabu kupitia kundi la TVR, nimejifunza mengi mno, nimekuwa nasoma vitabu vingine nje ya kundi lakini ndani ya kundi najifunza mengi zaidi.
Nichukue nafasi hii kuwashukuru sana marafiki ambao tumekuwa kwenye kundi pamoja kwa kipindi hiki. Kwa kipekee niwashukuru viongozi wa kundi, Deo Kessy, Daudi Mwakalinga na Daudi Siwalaze. Wameweza kuendesha kundi vizuri kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, na tunazidi kupata na kushirikishana maarifa haya muhimu ya kuyaboresha maisha yetu zaidi.
Hapo chini nimeorodhesha vitabu 105 tulivyovisoma mwaka 2016 kwenye kundi letu hili. Unaweza kuvipitia na kujionea mwenyewe.
Karibu uwe mwanachama wa kundi hili la kusoma vitabu.
Nawe pia unaweza kuwa mwanachama wa kundi hili la kusoma vitabu. Sifa pekee unazohitaji ni uweze kusoma Kiingereza, maana vitabu vingi ni vya Kiingereza, uwe tayari kusoma vitabu na kila Jumamosi jioni, kuanzia saa 12 jioni, uwe tayari kuwashirikisha wanakikundi mambo 20 uliyojifunza kutoka kwenye kila kitabu ulichosoma.
Kama unaona una sifa hizo na unapenda kweli kusoma vitabu, basi tuma ujumbe kwa njia ya TELEGRAM, telegram ni mtandao unaofanana na wasap, unaweza kuwa nao kwenye simu yako au hata kompyuta yako. Tuna ujumbe kwa mwenyekiti wa kundi hili, Bwana Deo Kessy, kwenye namba 0717 101 505. Mtumie ujumbe kwamba unapenda kujiunga na kundi la kusoma vitabu na umekubaliana na masharti ya kundi, kisha atakuweka kwenye kundi.
ANGALIZO KABLA HUJATUMA MAOMBO YAKO.
Hakikisha upo tayari kusoma vitabu, kwenye hili kundi hatuna biashara nyingine zaidi ya vitabu, na usipotimiza hilo unaondolewa, hakuna sababu sababu. Hivyo kama unaomba kujiunga, siku ukitolewa kwa sababu husomi vitabu na kuwashirikisha wengine, usianze kuleta malalamiko. Nasema hili kwa sababu watu wengi wakitolewa ndiyo wanakuja na malalamiko mengi.
Karibu sana rafiki kama upo tayari kuongeza maarifa zaidi. Lengo letu la kufika vitabu 500 tutalifikia bila shida, na tutakwenda zaidi na zaidi.
VITABU 105 TULIVYOSOMA KWENYE TVR MWAKA 2016.
1. 50 Great Lessons from Life - Tony O’Reilly
2. First things first - Sheila Mulcahy et al
3. 10X Rule-The Only Difference Between Success and Failure - Grant Cardone
4. The DNA of relationships - Dr. Gary Smalley
5. The Master Of Destiny - James Alen
6. Are You Fully Charged - Tom Rath
7. A More Beautiful Question-Power of Inquiry to spark breakthrough Ideas - Warren Berger
8. The Four Purposes of Life-Finding Meaning and Direction in a changing world - Dan Millman
9. Why Motivating People doesnt work - Susan Fowler
10. Critical Thinking - Halvey Segler
11. You Can Win - Shiv Khera
12. Simplicity Parenting - Kim John Payne and Lisa M. Ross
13. Innovation-Small book about Big ideas - Max McKeown
14. The Confidence Game- Maria Kannikova
15. Don’t Go Back To School - Kio Stark
16. In Good Times and Bad - Gary and Melisa Neuman
17. Young World Rising - Rob Salkowitz
18. The Book of Life - Krishnamurti Jiddu
19. How to become Genius and Expert in any subject with Accelarated Learning - Harvey Segle
20. The Naked Millionaire - David Taylor
21. All Time Essentials for Entrepreneurs - Jonathan Yate
22. Managing Oneself - Peter Ferdinand Drucker
23. Handbook to higher Consciousness - Ken Keyes
24. Zen to Done-The Ultimate Simple Productivity System - Leo Babauta
25. The hard truth about Soft Skills - Peggy Klaus
26. My Philosophy for Successful Living - Jim Rohn
27. Difficult Conversation-How to discuss what matters most - Douglas Stone, Bruce Patton, Sheila Heen
28. Stunning Success - Robin Sharma
29. The Longevity Project - Dr Friedman
30. Ignore everybody and 39 other keys to Creativity - Hugh Macleod
31. SpeedWealth - T. Harv Eker
32. 7 Habits of Highly Effective People - Stephen Covey
33. The Creator's Code-The Six Essential Skills of an Extraordinary Entrepreneur - Amy Wilkinson
34. The Family First-Your Step by Step Plan of Creating a phenomenal Family - Dr. Phil McGraw
35. The essentials of Business Entiquette - Barbara Pachter
36. Strengthfinder 2.0 - Tom Rath
37. The 50th Law - 50 Cent na Robert Greene
38. Lean In - Sheryl Sandberg
39. Deep Work - Cal Newport
40. Emotional Intelligence Works - Michael Ravitz and Susan Schubert
41. Failing Forward - John C. Maxwell
42. Happier - Tal Ben Shahar
43. The leader who had no title - Robin Sharma.
44. Men are from Mars, Women are from Venus - by John Gray
45. Smart Leaders-Smarter Teams - Roger Schwarz
46. Delivering Happiness - Tony Hsieh
47. Poke the Box - Seth Godin
48. Getting Results the Agile way - J.D. Meier
49. Just Listen - Mark Goulston
50. How to turn thoughts into Things - Bo Sanchez
51. The Lost Sven Secrets of Success - Joe Vitale
52. The Wonder Weeks - Hetty Van De Rijt, Frans Plooij
53. You were born Rich - Bob Proctor
54. Sign-posts on the road to Success - W.E Kenyon
55. Start with Why - Simon Sinek
56. The Way to Wealth - Benjamin Franklin
57. The Paradox of Choice-Why More is Less - Schwartz
58. Business at the Speed of Thought - Bill Gates
59. Tao Te Ching - Lao Tzu
60. 5 Love Languages of Children - Gary Chapman
61. Brain Storm: Tap into Your Creativity to Generate
Awesome Ideas and Remarkable Results - Jason Rich
62. The Defining Decade-Why your twenties matters - Meg Jay, PhD
63. How To Manage Your Boss - Ros Jay
64. Coach Yourself To Win - G. Huttman
65. Think Like a Champion - Donald Trump
66. Smart Leadership - Jonathan Yudelowitz
67. Eight Lessons for a Happier Marriage - William Glasser and Carleen
68. Blue Ocean Strategy - Kim Chan
69. Notes from a Friend - Anthony Robbins
70. Generation iY-Our Last Chance to Save their future - Tel Elmore
71. Be Your Own Brand - David and Karl D. Speak
72. Being Married - Sharon Aris
73. Secrets of The Richest Man Who ever lived - Mike Mudock
74. Entrepreneurship 101 - Donald Trump
75. Selfish reasons to have more kids - Bryan Caplan
76. Prosperity on Purpose - Justine Herald
77. The Righteous Mind - Haidt
78. One Minute Manager - K. Blanchard
79. It's not about the money - Bob Proctor
80. Rules for a knight - Ethan Hawke
81. The 21 Irrefutable Laws of Leadership - John C. Maxwell
82. The Most Successful Business in the World - Michael E. Gerber
83. Secrets of Self -Made Millionaires - Adam Khoo
84. Artificial Maturity-Helping Kids Meeting the Challenge of becoming Authentic
Adults - Tim Elmore
85. From Poverty to Power - James Allen
86. Invisible Gorilla - Christopher Chabris
87. 10- Minutes Toughness - Jason Selk
88. The Road To Character - David Brooks
89. What Winners Do to Win - Nick Joy
90. Love is a Mix Tape - Sheffield Rob
91. A Whole New Mind-WHY RIGHT BRAINERS WILL RULE THE FUTURE - Daniel H. Pink
92. Power of Thinking Without Thinking - Malcolm Gladwell
93. Alone Together - Sherry Turkle
94. Mountains beyond mountains - Trancy Kidder
95. The Total Money Make Over - Dave Ramsey
96. Mentored by a Millionaire - Steven Km Scrott.
97. Unleashing Power of Rubber bands - O.Nancy
98. Daring Greatly-How the Courage to Be Vulnerable Transpforms the Way we Live, Love, parent and Lead - Brene Brown
99. 7 Keys to 1000 Times More - Mike Mudock
100. Winning - Jack and Suzy Welch
101. Flash Foresight-How to seed the Invisible and Do the Impossible - Daniel Burrus
102. I AM MALALA - The Girl Who Stood Up for Education and was Shot by the
Taliban - Malala Yousafzai
103. Lead The Field - Earl Nightngale
104. Love Dare
105. Sometimes You Win Sometimes You Learn - John C. Maxwell
Kila la Kheri Rafiki Yangu.
Rafiki na Kocha wako,
Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA
MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku.
Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)
Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na
kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.