Quantcast
Channel: AMKA MTANZANIA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1010

Vitabu 105 Tulivyosoma Kwenye Kundi La Kusoma Vitabu Kwa Mwaka 2016.

$
0
0

Rafiki,
Katikati ya mwaka 2014 nilipata maono (VISION) ya kusoma vitabu 500 ndani ya miaka mitano. Hakika haya yalikuwa maono makubwa ambayo sikuwahi kufikiri kama yanawezekana. Hivyo sikuanza kuyafanyia kazi mara moja, bali nilikaa chini nikifikiria inawezekanaje kufikia maono hayo makubwa. Mwenyewe nilipata wasiwasi kama itawezekana. Kwa wakati huo nilikuwa tayari nina miaka miwili ya usomaji wa vitabu, lakini sikuwa nimesoma vitabu vingi sana ndani ya miaka hiyo miwili.

Siku moja nikiwa na maongezi na rafiki yangu Daudi Mwakalinga nikamshirikisha hili, na akalipokea akawa chanya sana kwenye hili. Nikaona kumbe inawezekana. Basi nikakaa chini na kupiga mahesabu, vitabu 500 ndani ya miaka mitano vinaishaje? 

Nikagundua inabidi kusoma vitabu 100 kila mwaka, hivyo miaka mitano vitakuwa vitabu 500.

Nikaendelea na hesabu zangu, kama mwaka ninahitaji kusoma vitabu 100, je nitavigawaje hivyo vitabu 100. Nikaona kwa mwaka kuna wiki 52, hivyo kama nitasoma vitabu viwili kila siku, kwa mwaka vitakuwa vitabu 104, nikaona hapa sasa namba inahesabika. Vitabu viwili kila wiki, siyo mzigo mkubwa sana, angalau ni kitu kinachowezekana kufanyika.

Kufika Oktoba mwaka huo 2014 nilikuja na mpango wa kuanzisha kundi la kusoma vitabu, kwa sababu nilijua kama nataka kufikia lengo hili, basi ni vyema nikaenda na wale wanaoweza kwenda.

Kwa kuwa mimi huwa napenda kufanya mambo magumu yawe rahisi, nikasema inabidi kutengeneza kundi ambalo litakuwa na watu wanaopenda kusoma vitabu, na lisiongeze mzigo kwa mtu. Mfano ulazima wa kukutana mara kwa mara na mengine ambayo yangeweza kuzuia au kuleta changamoto kwenye usomaji wetu wa vitabu.

Hivyo nikaona njia rahisi ni kutumia teknolojia mpya zinazokuja kila siku. Hivyo nikaamua kuanzisha kundi kupitia mtandao wa TELEGRAM, wakati huo wasap ilikuwa bado hamwezi kutumiana vitabu, lakini telegram itafaa. Na nikaweka mpango kwamba tutakuwa na kundi la kusoma vitabu, ambapo shughuli pekee ni usomaji wa vitabu, na siku moja ya wiki kila mtu LAZIMA ashirikishe kile ambacho amesoma kwenye vitabu, na kwa kila kitabu ashirikishe mambo 20 aliyojifunza. Kushindwa kufanya hivyo zaidi ya wiki mbili mtu huyo anatolewa.

Basi baada ya kuona mpango huu ni mwema, ndipo nilipoandika na kutoa taarifa kwa watanzania wenzangu kupitia mtandao wa AMKA MTANZANIA. Nilijua taarifa hii ingepokelewa vizuri na kwa hamasa, lakini mambo yalikuwa tofauti. Wengi walisema haiwezekani, walipinga mno na kushangaa kabisa. lakini nashukuru kuna watu kama 50 kwa kipindi kile waliitikia wito na tukaanza kusoma vitabu.

Hapa ndipo TANZANIA VORACIOUS READERS() ilipozaliwa. Kundi la kusoma vitabu ambalo kila mtu anakaribishwa kujiunga bure kabisa, lakini asipotimiza wajibu wa kusoma vitabu na kushirikisha wengine yale aliyojifunza anaondolewa. Tangu kipindi hicho tumekuwa tunasoma vitabu viwili kila wiki na tumekuwa tunaongezeka na kupungua kulingana na watu kuweza kuendana na taratibu za kikundi.

Wapo watu walioondolewa kwenye kundi na kulalamika mno, na wakati utaratibu ulikuwa wazi kabisa kwamba usipotimiza mahitaji ya kundi la usomaji wa vitabu utaondolewa.

Ninachoweza kusema ni kwamba kwa zaidi ya miaka hii miwili ya kusoma vitabu kupitia kundi la TVR, nimejifunza mengi mno, nimekuwa nasoma vitabu vingine nje ya kundi lakini ndani ya kundi najifunza mengi zaidi.

Nichukue nafasi hii kuwashukuru sana marafiki ambao tumekuwa kwenye kundi pamoja kwa kipindi hiki. Kwa kipekee niwashukuru viongozi wa kundi, Deo Kessy, Daudi Mwakalinga na Daudi Siwalaze. Wameweza kuendesha kundi vizuri kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, na tunazidi kupata na kushirikishana maarifa haya muhimu ya kuyaboresha maisha yetu zaidi.

Hapo chini nimeorodhesha vitabu 105 tulivyovisoma mwaka 2016 kwenye kundi letu hili. Unaweza kuvipitia na kujionea mwenyewe.

 Karibu uwe mwanachama wa kundi hili la kusoma vitabu.

Nawe pia unaweza kuwa mwanachama wa kundi hili la kusoma vitabu. Sifa pekee unazohitaji ni uweze kusoma Kiingereza, maana vitabu vingi ni vya Kiingereza, uwe tayari kusoma vitabu na kila Jumamosi jioni, kuanzia saa 12 jioni, uwe tayari kuwashirikisha wanakikundi mambo 20 uliyojifunza kutoka kwenye kila kitabu ulichosoma.

Kama unaona una sifa hizo na unapenda kweli kusoma vitabu, basi tuma ujumbe kwa njia ya TELEGRAM, telegram ni mtandao unaofanana na wasap, unaweza kuwa nao kwenye simu yako au hata kompyuta yako. Tuna ujumbe kwa mwenyekiti wa kundi hili, Bwana Deo Kessy, kwenye namba 0717 101 505. Mtumie ujumbe kwamba unapenda kujiunga na kundi la kusoma vitabu na umekubaliana na masharti ya kundi, kisha atakuweka kwenye kundi.

ANGALIZO KABLA HUJATUMA MAOMBO YAKO.

Hakikisha upo tayari kusoma vitabu, kwenye hili kundi hatuna biashara nyingine zaidi ya vitabu, na usipotimiza hilo unaondolewa, hakuna sababu sababu. Hivyo kama unaomba kujiunga, siku ukitolewa kwa sababu husomi vitabu na kuwashirikisha wengine, usianze kuleta malalamiko. Nasema hili kwa sababu watu wengi wakitolewa ndiyo wanakuja na malalamiko mengi.

Karibu sana rafiki kama upo tayari kuongeza maarifa zaidi. Lengo letu la kufika vitabu 500 tutalifikia bila shida, na tutakwenda zaidi na zaidi.

VITABU 105 TULIVYOSOMA KWENYE TVR MWAKA 2016.

1. 50 Great Lessons from  Life -            Tony O’Reilly


2. First things first -  Sheila Mulcahy et al

3. 10X Rule-The Only Difference Between Success and Failure - Grant Cardone

4. The DNA of relationships - Dr. Gary Smalley

5. The Master Of Destiny - James Alen

6. Are You Fully Charged - Tom Rath

7. A More Beautiful Question-Power of Inquiry to spark breakthrough Ideas         - Warren Berger

8. The Four Purposes of Life-Finding Meaning and Direction in a changing world  - Dan Millman

9. Why Motivating People  doesnt work - Susan Fowler

10. Critical Thinking - Halvey Segler

11. You Can Win - Shiv Khera

12. Simplicity Parenting - Kim John Payne and Lisa M. Ross

13. Innovation-Small book about Big ideas - Max McKeown

14. The Confidence Game- Maria Kannikova

15. Don’t Go Back To School - Kio Stark

16. In Good Times and Bad - Gary and Melisa Neuman

17. Young World Rising - Rob Salkowitz

18. The Book of Life - Krishnamurti Jiddu

19. How to become  Genius and Expert in any subject with Accelarated Learning - Harvey Segle

20. The Naked Millionaire - David Taylor

21. All Time Essentials for Entrepreneurs - Jonathan Yate

22. Managing Oneself - Peter Ferdinand Drucker

23. Handbook to higher Consciousness - Ken Keyes

24. Zen to Done-The Ultimate Simple Productivity System - Leo Babauta

25. The hard truth about Soft Skills - Peggy Klaus

26. My Philosophy for Successful Living - Jim Rohn

27. Difficult Conversation-How to discuss what matters most - Douglas Stone, Bruce Patton, Sheila Heen

28. Stunning Success - Robin Sharma

29. The Longevity Project - Dr Friedman

30. Ignore everybody and 39 other keys to Creativity - Hugh Macleod

31. SpeedWealth - T. Harv Eker

32. 7 Habits of Highly Effective People - Stephen Covey

33. The Creator's Code-The Six Essential Skills of an Extraordinary Entrepreneur - Amy Wilkinson

34. The Family First-Your Step by Step Plan of Creating a phenomenal Family - Dr. Phil McGraw

35. The essentials of Business Entiquette - Barbara Pachter

36. Strengthfinder 2.0 - Tom Rath

37. The 50th Law - 50 Cent na Robert Greene

38. Lean In - Sheryl Sandberg

39. Deep Work - Cal Newport

40. Emotional Intelligence Works - Michael Ravitz and Susan Schubert

41. Failing Forward - John C. Maxwell

42. Happier - Tal Ben Shahar

43. The leader who had no title - Robin Sharma.

44. Men are from Mars, Women are from Venus - by John Gray

45. Smart Leaders-Smarter Teams - Roger Schwarz

46. Delivering Happiness - Tony Hsieh

47. Poke the Box - Seth Godin

48. Getting Results the Agile way - J.D. Meier

49. Just Listen - Mark Goulston

50. How to turn thoughts into Things - Bo Sanchez

51. The Lost Sven Secrets of Success - Joe Vitale

52. The Wonder Weeks - Hetty Van De Rijt, Frans Plooij

53. You were born Rich - Bob Proctor

54. Sign-posts on the road to Success            - W.E Kenyon

55. Start with Why - Simon Sinek

56. The Way to Wealth - Benjamin Franklin

57. The Paradox of Choice-Why More is Less - Schwartz

58. Business at the Speed of Thought - Bill Gates

59. Tao Te Ching - Lao Tzu

60. 5 Love Languages of Children - Gary Chapman

61. Brain Storm: Tap into Your Creativity to Generate
Awesome Ideas and Remarkable Results  - Jason Rich

62. The Defining Decade-Why your twenties matters - Meg Jay, PhD

63. How To Manage Your Boss - Ros Jay

64. Coach Yourself To Win - G. Huttman

65. Think Like a Champion - Donald Trump

66. Smart Leadership - Jonathan Yudelowitz

67. Eight Lessons for a Happier Marriage - William Glasser and Carleen

68. Blue Ocean Strategy - Kim Chan

69. Notes from a Friend - Anthony Robbins

70. Generation iY-Our Last Chance to Save their future - Tel Elmore

71. Be Your Own Brand - David and Karl D. Speak

72. Being Married - Sharon Aris

73. Secrets of The Richest Man Who ever lived - Mike Mudock

74. Entrepreneurship 101 - Donald Trump

75. Selfish reasons to have more kids - Bryan Caplan

76. Prosperity on Purpose - Justine Herald

77. The Righteous Mind - Haidt

78. One Minute Manager - K. Blanchard

79. It's not about the money - Bob Proctor

80. Rules for  a knight - Ethan Hawke

81. The 21 Irrefutable Laws of Leadership - John C. Maxwell

82. The Most Successful Business in the World - Michael E. Gerber

83. Secrets of Self -Made Millionaires - Adam Khoo

84. Artificial Maturity-Helping Kids Meeting the Challenge of becoming Authentic 
Adults - Tim Elmore

85. From Poverty to Power - James Allen

86. Invisible Gorilla - Christopher Chabris

87. 10- Minutes Toughness - Jason Selk

88. The Road To Character - David Brooks

89. What Winners Do to Win - Nick Joy

90. Love is a Mix Tape -  Sheffield Rob

91. A Whole New Mind-WHY RIGHT BRAINERS WILL RULE THE FUTURE - Daniel H. Pink

92. Power of Thinking Without Thinking - Malcolm Gladwell

93. Alone Together - Sherry Turkle

94. Mountains beyond mountains - Trancy Kidder

95. The Total Money Make Over - Dave Ramsey

96. Mentored by a Millionaire - Steven Km Scrott.

97. Unleashing Power of Rubber bands - O.Nancy

98. Daring Greatly-How the Courage to Be Vulnerable Transpforms the Way we Live, Love, parent and Lead - Brene Brown

99. 7 Keys to 1000 Times More            - Mike Mudock

100. Winning - Jack and Suzy Welch

101. Flash Foresight-How to seed the Invisible and Do the Impossible - Daniel Burrus

102. I AM MALALA - The Girl Who Stood Up for Education and was Shot by the 
Taliban - Malala Yousafzai

103. Lead The Field - Earl Nightngale

104. Love Dare

105. Sometimes You Win Sometimes You Learn - John C. Maxwell
                       
Kila la Kheri Rafiki Yangu.

Rafiki na Kocha wako,

Kama umejifunza kupitia makala hii karibu tujifunze zaidi kupitia KISIMA CHA 
MAARIFA, ambapo utaingia kwenye kundi la wasap na kupata mafunzo kila siku.  

Kwa kupata vitabu vya biashara na mafanikio tembelea MOBILE UNIVERSITY (bonyeza hayo maandishi.)

Pata kitabu BIASHARA NDANI YA AJIRA ujifunze jinsi unavyoweza kuanzisha na 
kukuza biashara yako, pia utajifunza mifereji nane(08) ya kipato unayopaswa kuwa nayo ili kufikia uhuru wa kifedha. Bonyeza maandishi haya kupata kitabu.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1010

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>