Habari rafiki?
Wiki iliyopita tuliendesha mafunzo ya kutengeneza fedha kwenye mtandao kwa kutumia blog. Tulijifunza mambo mengi na muhimu sana kupitia semina ile. Na mimi pia nilijifunza mengi kupitia maswali mbalimbali ambayo yalikuwa yanaulizwa na washiriki wa semina ile. Kupitia maswali yale, kuna kitu kimoja nimejifunza ambacho ni kikwazo kwa wengi kuanzisha na kukuza biashara zao. Katika makala hii tutaangalia kitu hicho kimoja na jinsi ya kuvuka kikwazo hiki ili kuwa na blog unayoweza kuitumia kutengeneza kipato.
Katika maswali mengi yaliyoulizwa na washiriki wa semina, swali moja lilikuwa linajirudia mara kwa mara. Swali hilo ni je nitaanzaje blog wakati bado sijafanya utafiti wa kutosha kwenye ile mada niliyochagua kuandikia? Kwa maana nyingine watu wengi wamekuwa wanafikiri kwamba inabidi usubiri na kujifunza sana mpaka ubobee ndiyo uweze kuwa na blog yako. Mwingine aliniambia kwamba kwa sasa anajifunza na kusoma vitabu vinavyohusiana na anachotaka kuandikia, hivyo akishakuwa tayari ndiyo ataanzisha blog.
Haya ni mawazo mazuri, lakini pia ni kikwazo kikubwa mno kwenye uanzishaji wa blog. Hii ni kwa sababu hakuna siku unayoweza kuamka na kusema leo nipo fiti kabisa, nimeshajua kila kitu na sasa naweza kuanzisha blog yangu. Nakuhakikishia siku hiyo haipo kabisa. Kila siku utajiona kuna kitu ambacho bado hujakijua vizuri, yaani kila siku kuna kitu cha kujifunza. Hivyo ukisema usubiri mpaka uwe tayari, utasubiri muda mrefu sana.
Changamoto nyingine kubwa ni kwamba vile unavyojifunza hubaki navyo kama vilivyo. Hii ina maana kwamba vingi unavyojifunza kila siku utavisahau, na hata kama utaandika mahali, bado kadiri siku zinakwenda utasahau. Utasahau vile vitu jinsi vilivyo lakini yale maarifa ya msingi utabaki nayo kwenye akili yako. Hivyo usifikiri kukisoma kitabu leo basi ndiyo umeshamaliza, siku siyo nyingi utasahau, hivyo utahitaji kukisoma tena, au kusoma vitabu vingine. Tangu nimeanza kusoma na kusikiliza vitabu, nimeshasoma na kusikiliza karibu vitabu 500, lakini siyo kwamba nakumbuka vitabu vyote karibu 500, ila yale maarifa ya msingi yaliyopo kwenye kitabu husika nakuwa nimeyabeba.
Hivyo basi rafiki yangu, ninachotaka kukuambia ni hiki, kama lengo lako ni kuwa na blog, basi wakati wa kuanzisha blog yako ni sasa, ni leo. Kama umeshajua ni vitu gani unataka kuandikia basi anzisha blog yako, hata kama hujafanya maandalizi ya kutosha.
Ukishakuwa na blog ndiyo itakusukuma ujifunze kwa sababu unahitaji kuikuza blog yako. Na kadiri unavyokuwa na wasomaji wengi, ndivyo unavyozidi kusukumwa kujifunza na kuwapatia maarifa na taarifa bora. Kwa njia hii itakubidi ujifunze, tofauti na usipofungua kabisa na kusubiri uwe tayari, kwa sababu hutakuwa na cha kukusukuma kuwa tayari.
Hivi ndivyo ilivyo rafiki yangu, njia bora ya kujifunza kitu kwenye maisha ni kufanya, unajifunza mengi ukiwa unafanya kuliko unaposema unajiandaa. Pia nimekuwa nawaambia watu unaweza kuanza ukiwa unafikiria utaandika vitu fulani, lakini kadiri unavyokwenda ukajikuta unabadilika kulingana na taarifa unazokuwa unapata kila siku na wasomaji ulionao.
Hivyo rafiki yangu, kama unataka kuwa na blog, kuwa nayo leo au hutokuja kuwa nayo kabisa. Kuwa nayo leo kwa kuchagua kuanzisha blog na kuendelea kujifunza kadiri siku zinavyokwenda, au jiambie kwa sasa unajiandaa na utajiandaa maisha yako yote. Nawajua watu wengi ambao wanajiandaa kila siku na hawakaribii kuanza. Anza sasa na hayo mengine utajifunza kadiri siku zinavyokwenda.
MUHIMU;
Ofa ya kupata kitabu cha JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA KWENYE MTANDAO KWA KUTUMIA BLOG inaisha ijumaa tarehe 30/09/2016. Kitabu hiki kinakufundisha hatua kwa hatua jinsi unavyoweza kutengeneza blog yako mwenyewe na kuikuza hatimaye kutengeneza kipato. Utakipata kitabu hiki kwa sasa kwa tsh elfu 5 tu, baada ya muda wa ofa kuisha bei itaendelea kuwa ya kawaida tsh elfu 10. Kupata kitabu hiki tuma fedha tsh elfu 5 kwenye namba 0717 396 253 au 0755 953 887 kisha tuma email yako na utatumiwa kitabu.
Kuna nafasi ya kujiunga na kundi la wasap la PROFFESIONAL BLOGGERS, huku utajifunza mengi katika kuanzisha na kukuza blog yako. Pia utapata nafasi ya kuniuliza swali lolote kuhusu blog. Kujiunga na kundi hili unatakiwa kulipa ada ya tsh elfu 5 kila mwezi. Kujiunga tuma ujumbe kwa njia ya wasap kwenda namba 0717 396 253.
Pia kuna nafasi ya kuwa na blog ya kitaalamu kwenye mtandao wa MTAALAMU. Hapa unapata blog unayoweza kuitumia kukuza hadhira yako na baadaye kuigeuza kuwa sehemu ya kutengeneza kipato. Kwa kujiunga na mtandao huu unapata blog rahisi na iliyokamilika, email list, email yako maalumu na coaching kwenye swala la blogging. Kujiunga na mtandao huu tuma ujumbe kwa njia ya wasap kwenda namba 0717 396 253.
Karibu sana rafiki, kama unapata msukumo wa kuwa na blog ndani yako, basi kitu kimoja naweza kukuambia ni anza blog yako leo, hakuna siku bora kuliko leo na hakuna wakati utakuwa tayari kwa kila kitu. Anza na utakuwa unajifunza kadiri siku zinavyokwenda.
Rafiki na kocha wako,
Makirita Amani,
www.mtaalamu.net
Wiki iliyopita tuliendesha mafunzo ya kutengeneza fedha kwenye mtandao kwa kutumia blog. Tulijifunza mambo mengi na muhimu sana kupitia semina ile. Na mimi pia nilijifunza mengi kupitia maswali mbalimbali ambayo yalikuwa yanaulizwa na washiriki wa semina ile. Kupitia maswali yale, kuna kitu kimoja nimejifunza ambacho ni kikwazo kwa wengi kuanzisha na kukuza biashara zao. Katika makala hii tutaangalia kitu hicho kimoja na jinsi ya kuvuka kikwazo hiki ili kuwa na blog unayoweza kuitumia kutengeneza kipato.
Katika maswali mengi yaliyoulizwa na washiriki wa semina, swali moja lilikuwa linajirudia mara kwa mara. Swali hilo ni je nitaanzaje blog wakati bado sijafanya utafiti wa kutosha kwenye ile mada niliyochagua kuandikia? Kwa maana nyingine watu wengi wamekuwa wanafikiri kwamba inabidi usubiri na kujifunza sana mpaka ubobee ndiyo uweze kuwa na blog yako. Mwingine aliniambia kwamba kwa sasa anajifunza na kusoma vitabu vinavyohusiana na anachotaka kuandikia, hivyo akishakuwa tayari ndiyo ataanzisha blog.
Haya ni mawazo mazuri, lakini pia ni kikwazo kikubwa mno kwenye uanzishaji wa blog. Hii ni kwa sababu hakuna siku unayoweza kuamka na kusema leo nipo fiti kabisa, nimeshajua kila kitu na sasa naweza kuanzisha blog yangu. Nakuhakikishia siku hiyo haipo kabisa. Kila siku utajiona kuna kitu ambacho bado hujakijua vizuri, yaani kila siku kuna kitu cha kujifunza. Hivyo ukisema usubiri mpaka uwe tayari, utasubiri muda mrefu sana.
Changamoto nyingine kubwa ni kwamba vile unavyojifunza hubaki navyo kama vilivyo. Hii ina maana kwamba vingi unavyojifunza kila siku utavisahau, na hata kama utaandika mahali, bado kadiri siku zinakwenda utasahau. Utasahau vile vitu jinsi vilivyo lakini yale maarifa ya msingi utabaki nayo kwenye akili yako. Hivyo usifikiri kukisoma kitabu leo basi ndiyo umeshamaliza, siku siyo nyingi utasahau, hivyo utahitaji kukisoma tena, au kusoma vitabu vingine. Tangu nimeanza kusoma na kusikiliza vitabu, nimeshasoma na kusikiliza karibu vitabu 500, lakini siyo kwamba nakumbuka vitabu vyote karibu 500, ila yale maarifa ya msingi yaliyopo kwenye kitabu husika nakuwa nimeyabeba.
Hivyo basi rafiki yangu, ninachotaka kukuambia ni hiki, kama lengo lako ni kuwa na blog, basi wakati wa kuanzisha blog yako ni sasa, ni leo. Kama umeshajua ni vitu gani unataka kuandikia basi anzisha blog yako, hata kama hujafanya maandalizi ya kutosha.
Ukishakuwa na blog ndiyo itakusukuma ujifunze kwa sababu unahitaji kuikuza blog yako. Na kadiri unavyokuwa na wasomaji wengi, ndivyo unavyozidi kusukumwa kujifunza na kuwapatia maarifa na taarifa bora. Kwa njia hii itakubidi ujifunze, tofauti na usipofungua kabisa na kusubiri uwe tayari, kwa sababu hutakuwa na cha kukusukuma kuwa tayari.
Hivi ndivyo ilivyo rafiki yangu, njia bora ya kujifunza kitu kwenye maisha ni kufanya, unajifunza mengi ukiwa unafanya kuliko unaposema unajiandaa. Pia nimekuwa nawaambia watu unaweza kuanza ukiwa unafikiria utaandika vitu fulani, lakini kadiri unavyokwenda ukajikuta unabadilika kulingana na taarifa unazokuwa unapata kila siku na wasomaji ulionao.
Hivyo rafiki yangu, kama unataka kuwa na blog, kuwa nayo leo au hutokuja kuwa nayo kabisa. Kuwa nayo leo kwa kuchagua kuanzisha blog na kuendelea kujifunza kadiri siku zinavyokwenda, au jiambie kwa sasa unajiandaa na utajiandaa maisha yako yote. Nawajua watu wengi ambao wanajiandaa kila siku na hawakaribii kuanza. Anza sasa na hayo mengine utajifunza kadiri siku zinavyokwenda.
MUHIMU;
Ofa ya kupata kitabu cha JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA KWENYE MTANDAO KWA KUTUMIA BLOG inaisha ijumaa tarehe 30/09/2016. Kitabu hiki kinakufundisha hatua kwa hatua jinsi unavyoweza kutengeneza blog yako mwenyewe na kuikuza hatimaye kutengeneza kipato. Utakipata kitabu hiki kwa sasa kwa tsh elfu 5 tu, baada ya muda wa ofa kuisha bei itaendelea kuwa ya kawaida tsh elfu 10. Kupata kitabu hiki tuma fedha tsh elfu 5 kwenye namba 0717 396 253 au 0755 953 887 kisha tuma email yako na utatumiwa kitabu.
Kuna nafasi ya kujiunga na kundi la wasap la PROFFESIONAL BLOGGERS, huku utajifunza mengi katika kuanzisha na kukuza blog yako. Pia utapata nafasi ya kuniuliza swali lolote kuhusu blog. Kujiunga na kundi hili unatakiwa kulipa ada ya tsh elfu 5 kila mwezi. Kujiunga tuma ujumbe kwa njia ya wasap kwenda namba 0717 396 253.
Pia kuna nafasi ya kuwa na blog ya kitaalamu kwenye mtandao wa MTAALAMU. Hapa unapata blog unayoweza kuitumia kukuza hadhira yako na baadaye kuigeuza kuwa sehemu ya kutengeneza kipato. Kwa kujiunga na mtandao huu unapata blog rahisi na iliyokamilika, email list, email yako maalumu na coaching kwenye swala la blogging. Kujiunga na mtandao huu tuma ujumbe kwa njia ya wasap kwenda namba 0717 396 253.
Karibu sana rafiki, kama unapata msukumo wa kuwa na blog ndani yako, basi kitu kimoja naweza kukuambia ni anza blog yako leo, hakuna siku bora kuliko leo na hakuna wakati utakuwa tayari kwa kila kitu. Anza na utakuwa unajifunza kadiri siku zinavyokwenda.
Rafiki na kocha wako,
Makirita Amani,
www.mtaalamu.net