Quantcast
Channel: AMKA MTANZANIA
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1010

Pata Blog Yako Ya Kitaalamu Unayoweza Kutumia Kutengeneza Fedha Kwenye Mtandao, Soma Hapa.

$
0
0
Habari rafiki?
Wiki iliyopita niliendesha semina ya KUTENGENEZA FEDHA KWENYE MTANDAO KWA KUTUMIA BLOG. Zaidi ya marafiki 1000 walishiriki semina ile na wengi wamekiri kujifunza mambo mengi na makubwa. Kama ulikosa semina hii nzuri sana pole rafiki, lakini bado ipo njia ya wewe kunufaika na mafunzo yale niliyoyatoa. Na hapa nitakushirikisha njia unazoweza kutumia mpaka kumiliki blog yako mwenyewe ambayo utaitumia kutengeneza fedha kwenye mtandao. Katika mipango hii pia nitakupa nafasi ya kuendelea kuwa karibu na mimi ili tujifunze kwa pamoja. Soma hapa rafiki kisha uchukue hatua. Karibu sana.
Naomba nichukue nafasi hii kukupa mipango madhubuti ya kuweza kuanzisha na kukuza blog yako.


Mpango wa kwanza; Tangeneza blog yako mwenyewe ya bure.
Hapa ni wewe kutengeneza blog yako ya bure ambayo hutahitaji kuilipia tena. Na unahitaji maelekezo ya hatua kwa hatua ili kuweza kufanya hivyo. Nimeandika kitabu kinaitwa JINSI YA KUTENGENEZA FEDHA KWENYE MTANDAO KWA KUTUMIA BLOG. Kwenye kitabu hiki nimeonesha kwa njia ya picha hatua zote unazoweza kufuata na kuwa a blog yako mwenyewe ndani ya muda mfupi. kitabu hiki kinauzwa tsh elfu kumi na ni soft copy, kinatumwa kwa njia ya email.
Lakini kwa sababu wewe rafiki yangu umeshiriki semina hii ya blog, na napenda ukamilishe blog yako, nitakupa kitabu hiki kwa tsh elfu tano tu (5,000/=), kupata kitabu hiki tuma fedha tsh elfu tano kwa MPESA 0755 953 887 au TIGO PESA/AIRTEL MONEY 0717 396 253 kisha tuma email yako kwenye moja ya namba hizo pamoja na jina la kitabu na nitakutumia kitabu hicho mara moja. Ofa hii ya kupata kitabu cha blog kwa tsh elfu tano inaisha ijumaa tarehe 30/09/2016 hivyo chukua hatua sasa kama kweli unataka kuwa na blog nzuri.
Pia kitabu hiki kitakuwa kama rejea nzuri kwako, utakuwa na maarifa bora sana ya kufanyia kazi. Jipatie kitabu hiki leo.

Mpango wa pili; pata blog ya kitaalamu kwa ajili ya kuandika na kukuza hadhira yako.
Nimeandaa mpango maalumu kwa wale ambao hawataki kujihusisha kabisa na utengenezaji wa blog, tayari wao wana ujumbe wanataka kutoa au maarifa wanataka kuwashirikisha wengine lakini swala la kutengeneza na kurekebisha blog zao wenyewe hawaliwezi, na hawataki kujisumbua.
Nimetengeneza mtandao maalumu wa blog ambazo lengo lake ni kutoa maarifa na kufundisha, kuwafikia watu wengi na kuweza kutengeneza hadhira ya wasomaji. Blog hizi zitakuwa chini ya mtandao wa www.mtaalamu.net hii ina maana kwamba utakuwa na blog yako ambayo inaanza na mtaalamu.net, pia utakuwa na emaila yako inayoishia na mtaalamu.net kwa mfano blog yangu kwenye mtandao huu wa mtaalamu ni www.mtaalamu.net/makirita hapo nitaendelea kuwa nakushirikisha mambo mbalimbali kuhusu kutengeneza fedha kwa kutumia blog. Pia email yangu kwa mtandao huu ni makirita@mtaalamu.net

Kwa kujiunga na mtandao huu unapata blog yako ambayo inaanza na mtaalamu.net blog itakuwa na mwonekano rahisi (simple) na kusudi kubwa ni kuandika na kukuza hadhira. Pia utapata email yako ambayo utaweza kuitumia kwa mawasiliano na hata kuitumia kwenye email list yako. Utaunganishiwa blog yako na mitandao ya kijamii unayotumia, hivyo ukipost moja kwa moja inaenda kwenye mitandao hiyo. Na pia utatengenezewa na kuunganishiwa email list yako kwenye blog yako ili uweze kuikuza kupitia wasomaji wako.
Kupitia mtandao huu kazi yako itakuwa moja, kutoa maarifa na kukuza blog yako kuwafikia wengi, hizo kazi nyingine za kuhakikisha blog ipo hewani utaniachia mimi.

Unaweza kupata mfumo huu wa blog kwa kujiunga na kuwa unalipa ada ya tsh elfu 10 tu kila mwezi. Ni ada ambayo itakupa mengi na mazuri. Pia kwa kuwa na blog kwenye mtandao huu, utakuwa kwenye kundi maalumu la blog za wataalamu ambapo nitakuwa nawacoach bure kabisa. Nitakuwa nafuatilia blog ya kila mtu kwa ukaribu na kumhamasisha na kumshauri hatua bora za kuchukua.
Tuwasiliane sasa ili uweze kupata mpango huu wa blog, niandikie ujumbe kwa njia ya wasap kwenye namba 0717 396 253. Karibu sana.

Mpango wa tatu; karibu nikutengenezee blog yako mwenyewe kama unavyotaka iwe.
Kama unataka kuwa na blog yako nzuri na inayoendana na kile unachotaka, lakini huwezi kuitengeneza mwenyewe, naweza kukusaidia kufanya hivyo. Naweza kukutengenezea blog nzuri ambayo utaiendesha bure, ambayo itaishia blogspot.com au wordpress.com na pia naweza kukutengenezea blog nzuri ambayo unaimiliki mwenyewe, jina likaishia .com au .co.tz na ukawa na email zinazoendana na jina la blog yako. Blog ya kuendesha bure natengeneza kwa tsh elfu 50, ambapo unapata kila kituna blog ya kumiliki wewe mwenyewe natengeneza kwa tsh 300,000/= na kila mwaka utakuwa unalipia tsh 150,000/= kwa ajili ya jina la blog (domain name) pamoja na sehemu ya kuihifadhi kwenye mtandao (hosting space). Hapa utapata blog inayoendana na kile unachokitaka.

Pia kama utahitaji domain pekee au hosting ya blog yako tuwasiliane. Karibu sana kama utahitaji nikutengenezee blog yako pamoja na kuendelea kkushauri, nipigie simu kwenye namba 0717 396 253.

Mpango wa nne; karibu ujiunge kwenye kundi maalumu la wasap la PROFFESIONAL BLOGGERS.
Kama nilivyosema, kuwa mwenyewe ni rahisi sana kukata tamaa na kuishia njiani. Lakini ukiwa na kikundi cha watu ambao mnakwenda pamoja, inakuwa rahisi kupata hamasa na kuendelea hata pale unapokutana na changamoto au vikwazo. Pia itakuwa njia rahisi ya kuendelea kujifunza kila siku, kuuliza maswali pale ambapo unakutana na ugumu na kupata majibu ya kufanyia kazi.

Nimeanzisha kundi maalumu la bloggers nimeliita PROFFESIONAL BLOGGERS, kundi hili lipo kwenye wasap na linapokea watu wote ambao wameshaanzisha blog, au wana mpango wa kuanzisha blog. Katika kundi hili nitafundisha mengi ikiwa ni pamoja na uandishi wa makala zenye mvuto na kuhamasisha watu kuchukua hatua. Kujiunga na kundi hili unatakiwa kulipa ada ya kila mwezi ambayo ni tsh elfu 5 (5,000/=) pekee. Hiki ni kiasi kidogo sana ukilinganisha na thamani kubwa utakayoipata ukiwa kwenye kundi hilo, na hapo unakuwa na nafasi ya kuweza kuniambia nitembelee blog yako na kukushauri zaidi.
Kwa wale ambao watakuwa wamejiunga na mtaalamu.net na kuwa na blog zao pale, hawatahitaji kulipa ada hii ya elfu tano, badala yake wataendelea kulipa ada ta tsh elfu kumi ili kuwa na blog zao za kitaalamu.

Kwenye kundi hili la wasap, nitakusaidia kuijengea nidhamu ya uandishi kama bado huna, maana hii ndiyo inawaangusha wengi.
Kujiunga na kundi hili, tuma ada ya mwezi tsh elfu tano kwa MPESA 0755 953 887 au TIGO PESA/AIRTEL MONEY 0717 396 253 kisha tuma ujumbe kwa njia ya wasap kwenda namba 0717 396 253 wenye majina yako kamili na ujumbe kwamba unataka kuunganishwa kwenye kundi la PROFESSIONAL BLOGGERS. Karibu sana tuwe karibu.

Hii ndiyo mipango minne ya kuweza kukusaidia kusimama na blog yako. Chagua mpango wa blog utakaokufaa, kama ni kutengeneza blog yako mwenyewe, kuwa na blog kwenye mtandao wa mtaalamu (kitu ambacho nashauri sana) au nikutengenezee blog yako.
Kwa mpango wowote unaochagua, hakikisha unaingia kwneye kundi la wasap la PROFESSIONAL BLOGGERS, hapo ndipo elimu hii itakuwa inaendelea kila siku na maswali yako yatajibiwa kwa uhakika.

Karibu sana tufanye kazi pamoja, nikushirikishe kila ninachojua na kila ninachoendelea kujifunza.
Rafiki na Kocha wako,
Makirita Amani,
makirita@kisimachamaarifa.co.tz
www.kisimachamaarifa.co.tz

Viewing all articles
Browse latest Browse all 1010

Trending Articles